Bila P-Funk, Marco Chali, Pancho nisingeiva kama producer – Dully Sykes

 Dully
Dully Sykes amemtaja producer wa Bongo Records, P-Funk Majani kuwa ni miongoni mwa watu waliomfundisha mambo mengi kuhusiana na utayarishaji wa nyimbo.

Dully aliwahi kumiliki studio iitwayo Dhahabu Records kabla ya kuanzisha nyingine 4.12 iliyopo hadi sasa ambapo yeye mwenyewe ndiye producer.
“Namshukuru sana P-Funk maana yeye ndo kati ya maproducer walionisaidia na kunifundisha hata kugonga kick na snare,” Dully aliiambia E-News ya EATV.
“Alikuwa ananiambia kuwa kiCi inatakiwa KUWA katika level ipi ili muziki usikike vizuri, yaani namshukuru amenifundisha vingi. Na mtu kama Marco Chali alikuwa sio mchoyo kunipa vitu. Namshukuru pia Pancho ni mdogo wangu nimemlea mwenyewe na Producer Mbezi, hawa ni wadogo zangu wamenisaidia sana.”

0 Response to "Bila P-Funk, Marco Chali, Pancho nisingeiva kama producer – Dully Sykes"

Chapisha Maoni