Wanaume mnajua hili: Mfanyie mwanamke mautundu haya akuzidishie raha


MAMBO vipi ndugu zangu? Ni furaha yangu kwa mara nyingine tena kukutana nanyi wapendwa wasomaji wa safu yetu hii. Tumshukuru Muumba wetu kwa kutujaalia uhai na afya njema, lakini zaidi ya hapo tumshukuru pia kwa kutuumbia kitu mapenzi au siyo jamani?
Siku zote hatutaacha kuzungumza juu ya mapenzi kwani ni ukweli usiopingika kwamba mapenzi ndiyo maisha yetu.
Tunafanya kazi usiku na mchana, tunahangaika huku na huko, lakini mwisho wa siku tunafikiria jinsi gani tutapata kuboresha na kufurahia maisha na wapenzi wetu.
Tunafikiria pia ni jinsi gani tunaweza tukapata utulivu na amani katika maisha ya kimapenzi na wapenzi wetu, waume zetu au wake zetu katika siku zote za maisha yetu.
Ndugu zangu, Mungu ametuwekea mapenzi ili tupate raha na amani katika maisha yetu.
Kwa maana hiyo, wale wanaoyachezea na kuyavuruga mapenzi kwa makusudi kwa kuumiza hisia za wenzao kisha kuwasababishia vilio si watu wa kupendeza mbele ya macho ya wale wanaojua hasa nini maana ya mapenzi.
Wanawake ni watu wa kuheshimika na kupewa furaha wanayohitaji. Unapompata mwanamke anayekupenda na kukuheshimu, huna sababu ya kumfanya ajute kuwa na wewe.
MPENDE NA MTHAMINI!
Yawapasa wanaume mfahamu kuwa, wanawake ni zawadi kwenu, pumziko na tulizo la mioyo yenu. Wanawake ndiyo raha na amani kubwa ya maisha yenu.
Kosa kubwa mnalofanya wanaume ni kuutumia vibaya mfumo dume hasa katika suala nyeti kama mapenzi.  Mapenzi si ubabe, mapenzi ni upole na ukarimu.
 Pamoja na kwamba mmebarikiwa kwa kupewa nafasi ya kuwa kichwa katika nyumba lakini linapokuja suala la kurekebisha tofauti zinazojitokeza katika uhusiano wenu, si vyema kutumia njia za kibabe.
Niwaambie kitu, wanawake ni wa hisia zaidi na waliobarikiwa kuwa na upendo wa hali ya juu na ndiyo maana wakapewa dhamana ya kubeba mtoto tumboni kwa miezi tisa na pia kumnyonyesha na kumlea kwa miaka kadhaa, wewe mwanaume ungeweza?
Nasema ni watu wa hisia kwa sababu, hivi uliwahi kufikiri ni kwa nini wanawake huridhika na kujisikia poa kweli wanapopewa zawadi kama ya maua na kadi zenye ujumbe wa mapenzi ukilinganisha na wanaume?
Unafikiri ni kwa nini wana machozi ya haraka wanapotendwa? Au unafikiri ni kwa nini wanapenda kutumiwa ‘love sms’ zaidi kuliko kupigiwa simu? Jiulize.
Mimi nawaona wanawake kama watu wa kuheshimiwa na kupendwa kwa dhati.  Mkumbuke wanawake ndiyo mama zetu, walezi wetu na ndiyo nyumba zetu. Jaribuni pia kujicontroo na huo mnaouita ukijogoo kwamba eti ninyi ni watu msioridhika na mpenzi mmoja.
Jaribuni kufanya kila mnaloweza kuifuta ile dhana ya kwamba wanaume hawaaminiki hata kidogo. Ridhika na mpenzi uliyenaye, heshimu hisia zake na thamini mapenzi yake kwako na mpe ile kitu roho inapenda!
Ni hayo tu kwa leo.
MWIGIZAJI MZEE MANENTO KUZIKWA KESHO MOSHI-KILIMANJARO

MWIGIZAJI MZEE MANENTO KUZIKWA KESHO MOSHI-KILIMANJARO

MSIBA : Muigizaji Mzee Manento amefariki dunia.

NA SYLVESTER DAVID
MAZISHI ya msanii wa filamu za Kibongo, Mzee Manento yanatarajiwa kufanyika siku ya jumamosi nyumbani kwao mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na MUZIKI BEGANI Jana Jijini Dar es salaam,mmoja wasanii wa Bongo Movie anayetambulika kwa jina la, Robert Augustino maarufu kama Kiwewe alisema mwili wa marehemu utasafirishwa kwenda mkoani Kilimanjaro baada ya kuuaga rasmi jana nyumbani kwake kigogo.

Manento alifariki dunia juzi akiwa amelazwa katika hospitari ya TMJ iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya moyo kwa muda mrefu.

Mzee Manento atakumbukwa sana kwenye ulimwengu wa filamu nchini kutokana na kuonesha mchango mkubwa katika filamu za kibongo kama 'Hero of the Church', 'Dar to Lagos', 'Fake Pastor' na nyinginezo.

 Ndugu, jamaa na marafiki kwa sasa wamekutana nyumbani kwa marehemu kujadili kuhusu taratibu za kumsafirisha marehemu na utaratibu mzima wa mazishi.

Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi. AMEEN!


NEWZZZZZZZZ: MTANGAZAJI BEN KIKO AFARIKI DUNIA

NEWZZZZZZZZ: MTANGAZAJI BEN KIKO AFARIKI DUNIA



Ben Kiko enzi za uhai wake.
ALIYEKUWA mtangazaji maarufu wa Radio Tanzania, Ben Kiko, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Oktoba 31, 2014 akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akitibiwa.
Kiko amefariki baada ya kusumbuliwa na maradhi ya figo kwa muda mrefu.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN.
GADNER. G. HABASH ATUA RASMI EFM KWA KISHINDO

GADNER. G. HABASH ATUA RASMI EFM KWA KISHINDO

Mtangazaji  mahiri Gardner.G. Habash.
Mtangazaji  mahiri Gardner.G. Habash,amejiunga  na kituo cha Radio kinachokuja kwa kasi hivi sasa EFM 93.7  cha jijini Dsm ili kuongeza nguvu katika kikosi chao.

Akizungumza leo na waandishi wa habari afisa habari wa EFM Kanky Mwaigomole amesema wameamua kumchukua Gardner kwasababu ni miongoni mwa watangazaji hodari nchini mwenye kipaji cha hali ya juu hivyo kuongeza chachu ya mafanikio katika kituo hicho kipya.

“Gardner ataendesha kipindi kiitwacho Ubaoni kuanzia saa tisa alasiri mpaka saa moja kamili jioni kuanzia Jumatatu ya tarehe 03 mwezi wa 11 mwaka huu”alisema Kanky.

Gardner alimaarufu “KAPTENI” alianza kazi na kituo cha Radio Clouds fm na baadaye Times fm ambapo kwa sasa ametua Efm akitanguliwa na wakongwe kama Dj Majey,Dizzo One,Sos B,Denis Ssebo,Maulidi Kitenge,Omari Katanga,Scholastica Mazula na Kanky Mwaigomole.
Asante,
Meneja Uhusiano.
Kanky Mwaigomole.

Wolper alijia juu gazeti baada ya gazeti kumwandika eti amekua akimtumia picha za utupu Ali kiba

                                          

Wolper alijia Juu gazeti  moja hapa  mjini baada ya gazeti kumuwandika eti amekua akimtumia picha za utupu Ali kiba.Wolper andika hivi kwenye account yake ya Instagram,tazama hapo chini