Sheddy Clever Atangaza Ndoa Baada ya Kumtambulisha Mpenziwe


Si watu maarufu wengi wanaweka wazi mahusiano yao kwa malengo na faida binafsi au za kikazi zaidi. Imetokea mara kadha mastaa hapa nchini na duniani kuwa wazi kwa mapenzi yao kwa kuwatambulisha kupitia hata katika mitandao ya kijamii na kwingineko na wengine kuficha kuto taka hata kidogo kufahamika katika mahusiano yao.
Kushoto ni mpenzi wa Sheddy Clever akiwa na kipenzi chake producer Sheddy. Sheddy Clever ni producer mwenye umaarufu mkubwa nchini na duniani hasa baada ya kufanya kibao cha My Number One ya Diamond.
Ilikuwa katika onesho moja la aina yake na la kwanza kwa Sheddy kulifanya toka awe kwenye kilele cha tasnia ya wazalishaji wa mziki wa Tanzania, kupitia onesho hilo "USIKU WA SHEDDY" Ndipo mwishoni aliamua kumtambulisha mpenzi wake hasa kwa kuonesha upendo wake wa dhati kati yake na mpenziwe moja kwa moja katika jukwaa na kuahidi kumuoa hivi karibuni.
Kwa mabusu mwananaa walipongezana hadharani hiyo ilikuwa ni kuthibitisha kuwa hawana utani kabisa na mahusiano yao, ilikuwa raha kwao kwa kweli.
Mimer; Mrimbwende wa Producer Sheddy,